KIUT YAJIPANGA KUWEKEZA MPIRA WA WAVU

na VICTORIA GODFREY

UONGOZI wa Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala nchini Tanzania [KIUT] umesema utaendela kuwekeza ili kupata wachezaji wazuri katika mchezo wa wavu waweze kwenda kushindana kimataifa.

Hivi karibuni timu ya chuo hicho kwa mchezo wa mpira wa wavu wanawake na wanaume imeshiriki mashindano ya kimataifa yaliyopewa jina KAVC yaliyo malizika nchini Uganda.

Akizungumza na zanzibarleo rais wa michezo wa KIUT Peter Kaahwa, alisema kuendelea kusaka vipaji kwa kuwawezesha kimichezo na elimu  ya darasani.

Alisema lengo ni kuhakikisha wanaongeza nguvu katika kikosi kilichopo ili kiwe katika ushindani kwa mashindano ya ndani na nje ya Tanzania.

Naye meneja wa KIUT Mushabe Rogers, alisema wamejifunza ya nchi shiriki zilizofanya uwekezaji wa timu za vijana wadogo na kuwapa fursa ya kushiriki  na kuleta ushindi.

”Kwa kweli ushiriki wetu kimataifa imewaongezeka wachezaji wetu kujipima viwango vyao na wachezaji wa nchi nyingine, kwetu ni fursa ya kujifunza wanafanya nini ili kushinda,” alisema Rogers.

CHANZO: ZANZIBAR LEO – GAZETI

 

related

Search
Generic filters
Exact matches only

Having Trouble Applying? (je, unahitaji msaada wa kufanya maombi?)

Please fill in your details and one of our agents will contact you shortly.
(Tafadhali jaza hii fomu, moja wa wakala wetu atawasiliana nawe hivi punde)

NOTE : * Means Required (Lazima Ijazwe)

SiteLock